SiasaMarekani
Iran yasema italipiza kisasi ikiwa itashambuliwa na Marekani
31 Machi 2025Matangazo
Kiongozi huyo mkuu wa Iran amesema ikiwa Marekani inafikiria kuleta uchochezi ndani ya nchi hiyo kama ilivyokuwa miaka iliyopita, raia wa Iran watakabiliana nayo.
Iran yakataa kuingia katika mazungumzo ya moja kwa moja na Marekani kuhusu mpango wake wa nyuklia
Hapo jana, Trump alisisitiza tishio lake kwamba Iran itashambuliwa kwa mabomu ikiwa haitakubali pendekezo lake la mazungumzo yaliyoainishwa katika barua iliyotumwa kwa uongozi wa Iranmapema mwezi Machi, na kuipa nchi hiyo muda wa miezi miwili kufanya uamuzi.