MigogoroMashariki ya Kati
Iran yalaani vikali mashambulizi ya Israel nchini Yemen
6 Mei 2025Matangazo
Iran kupitia Msemaji wa wizara ya mambo ya nje Esmaeil Baqaei imesema mashambulizi hayo ya Israel ni uhalifu wa wazi na ukiukaji mkubwa wa kanuni na sheria za kimataifa.
Baqaei amezitaka mamlaka za kikanda na kimataifa kuchukua hatua dhidi ya kile alichokiita "uharibifu" unaoendelea wa Marekani na Israel katika nchi za Kiislamu.
Hayo yanajiri baada ya Wahouthi wanaoungwa mkono na Iran kushambulia kwa makombora uwanja mkuu wa ndege wa Israel mjini Tel Aviv na kuvuruga usafiri wa ndege.