SiasaIran
Iran yalaani marufuku ya kusafiri ya Marekani kwa Wairani
7 Juni 2025Matangazo
Alireza Hashemi-Raja, mkurugenzi mkuu wa masuala ya Wairani wanaoishi nje katika wizara ya mambo ya nje, ameitaja hatua hiyo, ambayo inaanza kutekelezwa Juni 9, kuwa ni ishara ya wazi ya kushamiri kwa fikra za ubaguzi wa rangi na ubabe miongoni mwa watunga sera wa Marekani.
Aliongeza kuwa uamuzi huo unaonyesha chuki kubwa ya utawala wa Marekani dhidi ya watu wa Iran na chuki dhidi ya Uislamu.
Rais wa Marekani Donald Trump alitangaza Jumatano marufuku kali za usafiri ambazo alizitetea kwa misingi ya usalama wa taifa kufuatia shambulio la bomu katika maandamano ya kuunga mkono Israel huko Colorado.