Iran yakataa kuzungumza na Marekani kuhusu mpango wa nyuklia
30 Machi 2025Matangazo
Rais huyo amesema licha ya Iran kuondoa uwezekano wa pande hizo mbili kufanya mazungumzo ya moja kwa moja, bado milango yake iko wazi ya kujadiliana kupitia wawakilishi.
China na Urusi zaiunga mkono Iran wakati Trump akishinikiza mazungumzo ya nyuklia
Hata hivyo haijawa wazi iwapo Trump atakubali mazungumzo yasiokuwa ya moja kwa moja. Mazungumzo kama hayo yaliofanyika hapo nyuma, tangu mwaka 2018 wakati Trump alipoiondoa Marekani kwenye mkataba wa nyuklia kati ya Iran na madola yenye nguvu, uliofikiwa mwaka 2015, na kurejesha vikwazo vikali vya kiuchumi dhidi ya Iran, hayajawahi kufua dafu.
Israel na Marekani zimeonya hawatoiacha Iran kuwa na silaha za nyuklia.