Iran na Israel zatikiwa kutuliza mvutano kati yao
13 Juni 2025Matangazo
Iran imerusha droni 100 kuelekea Israel kujibu mashambulizi ya Israel ambapo kwa mujibu wa ripoti za vyombo vya habari vya Israel droni hizo zimezuiwa.
Iran yasema Israel itawajibishwa kwa kuishambulia
Msemaji wa jeshi la Israel amesema, nchi hiyo imefanya mashambulizi makubwa ya anga kwa kutumia ndege za kivita zipatazo 200 kuvilenga vinu vya nyuklia vya Iranusiku wa kuamkia leo ambapo vinu 100 vililengwa.
Wakati huo huo mamia ya safari za ndege zimefutiliwa mbali katika viwanja vya ndege vya Mashariki ya Kati kufuatia mashambulizi hayo ya Israel.