Esmail Baghaei: Iran haitoacha kurutubusha madini Urani
26 Mei 2025Matangazo
Mazungumzo kati ya Marekani na Iran yanalenga kutatua mzozo wa muda mrefu kuhusu nia ya Iran ya kudhibiti silaha za nyuklia. Pande zote mbili zimekuwa na misimamo mikali kuhusu urutubishwaji wa madini ya Urani kutoka Jamhuri hiyo ya kiislamu.
Esmail Baghaei amesema kama Marekani ina nia njema katika mazungumzo hayo, basi Iran pia itakuwa na matumaini, lakini kama mazungumzo yatajikita kuzuwia haki za Iran hayatafika kokote.
Duru ya tano ya mazungumzo ya Nyuklia ya Iran kuanza Rome
Ameongeza kuwa kwa sasa Iran, inasubiri jibu kutoka kwa mpatanishi Oman, ili kujua tarehe itakayofikiwa ya mazungumzo ya duru ya sita na Marekani kuhusu mpango wake huo wa nyuklia.