SiasaIndonesia
Indonesia yajitolea kuwahifadhi kwa muda Wapalestina
9 Aprili 2025Matangazo
Subianto amesema Indonesia iko tayari kuwasafirisha takriban watu 1,000 katika awamu ya kwanza, kwa ndege maalum, na kuwahifadhi hadi wapone na hadi Gaza itakapokuwa na utulivu lakini akisisitiza hatua hiyo sio makazi ya kudumu.
Soma pia: Mashambulizi ya Israel leo yaua watu 25 huko Gaza
Kauli ya Subianto inajiri kabla ya kuelekea Abu Dhabi, kwa ziara ya Mashariki ya Kati itakayompeleka pia Uturuki, Misri, Qatar na Jordan, ambako atazungumzia mpango huo wa kibinadamu.
Indonesia, taifa lenye Waislamu wengi zaidi duniani, limekuwa mshirika wa karibu wa Palestina kwa muda mrefu.