Indonesia na China zakubaliana kuimarisha ushiriano
25 Mei 2025Nchi hizo mbili ni washirika muhimu kiuchumi. Makampuni mengi ya China yamewekeza katika rasilimali za Indonesia katika miaka ya hivi karibuni hasa katika sekta ya madini ya Nickel.
Hata hivyo misimamo ya mataifa hayo mawili kuhusu shughuli za kimkakati katika bahari ya China na maeneo yaliyoko karibu na eneo hilo, ilitia doa mahusiano yao.
Xi aapa kuimarisha uhusiano wa kimkakati na Indonesia
Katika mkutano wake na rais wa Indonesia Prabowo Subianto, Li Qiang alisema nchi yake iko makini kuendeleza ushirikiano na taifa hilo la Kusini mwa Asia lililo na uchumi mkubwa.
"China iko tayari kufanya kazi na Indonesia...kuendeleza utamaduni wetu wa kirafiki na kuimarisha mshikamano wetu na ushirikiano," alisema Clip Li Qiang
Prabowo pia alisisitiza urafiki na ukaribu wa nchi yake na China.