MigogoroAsia
India yazipiga marufuku bidhaa zinazotoka Pakistan
3 Mei 2025Matangazo
Mamlaka hiyo imesema sababu za kufanya hivo ni kulinda sera ya umma na maslahi ya kiusalama ya taifa hilo. India imechukua hatua hiyo wakati nchi hizo mbili zikikabiliwa na mivutano iliyochochewa zaidi na shambulio baya katika jimbo la Kashmir zinaloligombea.
Soma zaidi:Vikosi vya India na Pakistan vyashambuliana katika jimbo la Kashmir
Katika mkasa huo wabeba silaha waliwavamia na kuwauwa watu 26 wengi wao watalii katika eneo la Pahalgam mwezi uliopita.
India inaishutumu Pakistan kuwa ilihusika kufanikisha tukio hilo suala ambalo Pakistan inalikanusha huku ikisisitiza kuwa ina ushahidi wa kutosha wa kiitelijensia kuwa India inataka kuivamia kijeshi ili kulipa kisasi.