BiasharaIndia
India, Marekani waendelea kuzungumza baada ya ushuru wa 25%
31 Julai 2025Matangazo
Kulingana na Rais Trump ushuru huo unaanza kutekelezwa wa siku ya Ijumaa.
Trump aidha alisema kupitia mtandao wake wa Truth Social kwamba wataitoza India ushuru wa ziada wa kuingiza bidhaa nchini humo kwa sababu imenunua mafuta nchini Urusi.
Hata hivyo, Trump aliwaambia waandishi wa habari baadae kuwa nchi hizo mbili bado ziko kwenye mazungumzo ya biashara licha ya ushuru huo uliopangwa kuanza hivi karibuni.
Serikali ya India ilisema baada ya tangazo hilo kwamba inalichukulia kwa tahadhari kubwa.