Miaka 80 tangu kukombolewa kwa kambi ya Auschwitz
27 Januari 2025Matangazo
Watu waliosalimika katika mauaji hayo wanatarajiwa kuwa sehemu kubwa ya maadhimisho yanayofanyika leo katika kambi hiyo huko Poland.
Viongozi mbalimbali kutoka mataifa 55 watashiriki kwenye kumbukumbu hizo wakiwemo Rais wa Ujerumani Frank Walter Steinmeier, Kansela Olaf Scholz, Mfalme Charles wa Uingereza, Mfalme Felippe wa 6 wa Uhispania, Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron, na Rais wa Baraza la Ulaya, Antonio Costa.
Soma pia:Auschwitz ilikuwa "mfumo wa viwanda kwa ajili ya kuua watu."
Kambi ya Auschwitz ilikombolewa Januari 27 mwaka 1945 na Kikosi cha Red Army cha jeshi la Kisovieti katika eneo ambalo sasa linafahamika kama mji wa Oświęcim, nchini Poland.