MigogoroSudan
ICC: Uhalifu dhidi ya ubinadamu unafanyika Darfur Magharibi
11 Julai 2025Matangazo
Taarifa hiyo imetolewa na naibu mwendesha mashtaka wa mahakama hiyo Nazhat Shameem Khan alipokuwa akilihutubia Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa na kueleza kwamba mateso ya raia huko Darfur yamefikia kiwango kisichokubalika kwa kukosa maji na chakula.
Shameem Khan amesema njaa imeongezeka huku hospitali, misafara ya misaada ya kibinadamu na miundombinu ya kiraia vikilengwa moja kwa moja. Naibu mwendesha mashtaka huyo wa ICC ametaja kuongezeka nchini Sudan kwa makundi yenye silaha na kukithiri kwa vitendo vya ubakaji, unyanyasaji wa kijinsia na utekaji nyara.
Vita vya Sudan vilivyoanza April mwaka 2023 vimesababisha vifo vya karibu watu 40,000 huku wengine milioni 13 wakigeuka kuwa wakimbizi.